Sunday, October 16, 2016

SITTA AREJEA NCHINI KUTOKA UJERUMANI ALIKOENDA KUTIBIWA MIGUU

Spika wa Bunge mstaafu, Samuel Sitta amerejea nchini kutoka Ujerumani alikokwenda kwa ajili ya matibabu ya miguu.

Septemba mwaka huu, Sitta alikwenda nchini humo baada ya kusumbuliwa na tatizo hilo.

Mmoja wa wanafamilia wa mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa waziri wa wizara mbalimbali serikalini, alimwambia mwandishi wa habari hizi kuwa hali yake inaendelea vizuri.

 Hata hivyo mimi siyo msemaji wa familia,” alisema mtoa habari huyo.

Alipotafutwa mke wa Sitta, Margaret ambaye alirithi ubunge wa Urambo kutoka kwa mumewe, alisema alikuwa benki na asingeweza kuzungumza  na simu.




Jiunge na hatukwamii.blogspot.com/ sasa

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video 



0 comments:

Post a Comment