Tuesday, April 18, 2017

Mjadala ndani ya Sports Extra kuhusu utata unaoendelea kufunika pointi 3 za Simba

Jana April 17, 2017 katika kipindi cha Sport Extra cha Clouds FM uliibuka mjadala mkubwa wakati Alex Luambano na Shaffih Dauda wakijadili kuhusu Kamati ya Katiba Sheria na Hadhi za wachezaji kukutana leo April 18, 2017 kwa ajili ya kupitia uamuzi uliofanywa na Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji wa ligi Tanzania maarufu kwa jina la Kamati ya saa 72.
Kamati hiyo inakutana kutokana na ombi la timu ya Kagera Sugar ambayo imeomba kupitiwa upya uamuzi uliofanywa na Kamati ya Saa 72 ambayo kwa mujibu wa kanuni, ilitoa matokeo mapya ya mchezo kati ya timu hiyo na Simba uliofanyika Aprili 2, mwaka huu huko Uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera.
Katika mchezo huo, Kagera Sugar ilishinda mabao 2-1, lakini Simba ilikata rufaa ikidai kuwa Kagera Sugar ilivunja kanuni ya 37 (4) ya Ligi Kuu ya Vodacom kwa kumchezesha mchezaji Fakhi Mohammed ambaye alidaiwa na Simba kuwa alikuwa na kadi tatu za njano katika mechi tofauti za Liku Kuu ya Vodacom. Hivyo, ikaadhibiwa kwa mujibu wa kanuni ya 37 (37) ambayo ilitoa pointi tatu na magoli matatu kwa Simba.
katika mjadala huo huo, liliibuka swali kwamba, kwanini masuala yanayovihusu vilabu vya Simba na Yanga ndio hutatuliwa kwa haraka kuliko vilabu vingine vya ligi kuu?
U-Simba na U-Yanga ndio unasababisha mambo mengi yanapindishwa hilo lazima tukubali, watu wengi wenye mahaba juu ya hizi timu wanatumia nafasi walizonazo kufanya maamuzi ambayo wakati mwingine yanakwenda kinyume na taratibu.
Jiulize kuna mashauri mangapi ya malalamiko na rufaa pale TFF? Mfano mzuri ni sakata la Ludovic, ni kamati hii ya katiba, sheria na hadhi za wachezaji ndio inatakiwa itoa uamuzi lakini ipo kimya hadi leo, lakini limetokea suala ambalo lina maslahi kwa vilabu vya Simba na Yanga kamati inakutana haraka kujadili.
Kwa nini suala la Ludovic pia lisijadiliwe leo na kutolewa maamuzi kwa haraka kama ilivyo kwa masuala yanayo vihusu vilabu vya Simba na Yanga?
Kwa nini vikao ni vingi wakati kanuni zipo? Suala la mchezaji kuwa na kadi tatu za njano au kutokuwa nazo ni la kikanuni vikao vingi vya kamati vinatoka wapi? Mechi ya Kagera Sugar na African Lyon ndiyo inayoleta utata kwa sababu ndiyo inayo mhukumu mchezaji huka kwamba ndiyo ilikuwa mechi ya tatu mfululizo anaoneshwa kadi ya njano. Mechi hiyo hiyo ndio Kagera wanasema mchezaji hakuoneshwa kadi lakini wanakubali kuwa kabla ya mechi hiyo ni kweli alikuwa na kadi mbili za njano.
Sawa wanasema mechi haikuoneshwa na Azam TV wala haikurekodiwa, hebu tujiulize maswali kadhaa hapa. Waamuzi wa mechi husika (Kagera Sugar vs African Lyon) wanasemaje? Taratibu zinasemaje kuhusu mwamuzi kutuma ripoti baada ya mechi kumalizika, je ripoti ilitumwa ndani ya muda?
Waamuzi wa hiyo mechi, fourth official pamoja na msimamizi wa kituo wanajua kama hiyo kadi ipo au haipo.
Kwa upande wao Kagera Sugar wanasema kwenye rekodi zao hakuna hiyo kadi inayolalamikiwa na Simba. Kwa utafiti uliofanywa kwa baadhi ya wachezaji wa African Lyon waliocheza mechi dhidi ya Kagera Sugar wanasema hawakuona tukio lolote alilofanya Mohamed Fakhi lililopelekea kuoneshwa kadi ya njano na hawakuona mwamuzi akimuopnesha Fakhi kadi ya njano.

source:shaffihdauda
Tuandikie Maoni Yako Hapa Chini. Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video za kufurahisha na kuvunja mbavu.

0 comments:

Post a Comment