Waziri Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye amesema
amesikia kilio cha wasanii kuhusu kuwabana katika kazi zao hususan
kwenye video za muziki na kuahidi kufumba jicho moja ili kuwapa uhuru
kiasi.

Ametoa ahadi hiyo wakati akizungumza kwenye tuzo za EATV zilizotolewa kwa mara ya kwanza Jumamosi hii kwenye ukumbi wa Mlimani City.
“Tutaachia kidogo hatutabana sana, “alisema Nape. “Na mimi nimepita mtaani naambiwa ‘Nape mmebana sana.’ Wakati mwingine tunataka kufanya mambo tunaambiwa tumepitiliza. Wakati mwingine tutafumba jicho moja watu wapitilize kidogo ili mambo yaende sawa sawa,” alisisitiza waziri huyo aliyekuwa mgeni rasmi kwenye tuzo hizo.
Kwa muda mrefu Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA lililo chini ya wizara yake, limekuwa likilaumiwa kwa kutoa adhabu kali kwa wasanii kwa kile inachosema ni kuvunja maadili.

Ametoa ahadi hiyo wakati akizungumza kwenye tuzo za EATV zilizotolewa kwa mara ya kwanza Jumamosi hii kwenye ukumbi wa Mlimani City.
“Tutaachia kidogo hatutabana sana, “alisema Nape. “Na mimi nimepita mtaani naambiwa ‘Nape mmebana sana.’ Wakati mwingine tunataka kufanya mambo tunaambiwa tumepitiliza. Wakati mwingine tutafumba jicho moja watu wapitilize kidogo ili mambo yaende sawa sawa,” alisisitiza waziri huyo aliyekuwa mgeni rasmi kwenye tuzo hizo.
Kwa muda mrefu Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA lililo chini ya wizara yake, limekuwa likilaumiwa kwa kutoa adhabu kali kwa wasanii kwa kile inachosema ni kuvunja maadili.
Source:bongo5
Jiunge na hatukwamii.blogspot.com/ sasa
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video
0 comments:
Post a Comment