HATIMAYE Rais John Magufuli ameweka bayana ukweli kuhusu uwekezaji wa
kiwanda cha saruji cha Dangote, mkoani Mtwara. Rais Magufuli amesema,
‘wapiga dili’ walitaka kujinufaisha kupitia mradi huo, lakini mbinu zao
zimeshindwa na sasa waliotaka kuukwamisha watakiona cha moto.
Rais Magufuli amemuhakikishia mmiliki wa kiwanda hicho, Aliko Dangote kuwa serikali itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji na kumtaka mmiliki huyo kununua gesi moja kwa moja kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), badala ya kutumia watu wenye nia ya kutengeneza faida binafsi.
Rais Magufuli alisema hayo jana Ikulu jijini Dar es Salaam wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Dangote na kusema hakukuwa na tatizo lolote la kiserikali baina ya mwekezaji huyo, bali kulikuwa na watu waliotaka kujinufaisha binafsi kupitia mradi huo.
“Hakuna tatizo lolote baina ya serikali na mmiliki wa kiwanda hiki, bali kulikuwa na watu waliotaka kujinufaisha binafsi kupitia mradi huu kwa kufanya biashara za ujanja ujanja jambo ambalo serikali haliruhusu, na tutawachukulia hatua wote,”alisema Rais Magufuli.
Alisema mradi huo uliingiliwa na wapiga dili wakiwemo wanasiasa na kusema serikali haitaruhusu michezo hiyo na kwamba mianya yao imefungwa na wote waliohusika kutaka kuuvuruga, watashughulikiwa na serikali.
Rais Magufuli alimueleza mmiliki huyo nia ya serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inatimiza malengo ya kuwa nchi ya viwanda na kuwa iwapo atataka maelezo yoyote au iwapo atakwamishwa ni vyema awasiliane na viongozi wa serikali badala ya kutumia watu ambao nia yao ni kutengeneza faida tu.
“Iwapo unataka maelezo yoyote ama lolote linalokukwamisha uwasiliane na viongozi wa serikali badala ya kuwasiliana na watu ambao wako kwa ajili ya kufanya biashara ya ujanja ujanja kwa lengo la kupiga dili,” alisema Rais Magufuli.
Alisema mmiliki huyo alitaka eneo dogo kwa ajili ya kusafirishia saruji yake ila walijitokeza watu ambao wametaka kumuuzia kwa shilingi bilioni 43, jambo ambalo halina uhalisia wowote bali ni watu wenye nia ya kutaka faida na kusema jambo hilo haliwezekani katika serikali yake.
Akizungumzia hilo la eneo, Rais alisema wapo watu waliosikia Dangote anataka kununua eneo hilo dogo kwa ajili ya kusafirisha saruji na wao wakakimbilia kununua maeneo hayo na kutaka wamuuzie kwa bei kubwa, jambo ambalo alisema halikubaliki hata kidogo.
Kuhusu gesi Rais alimtaka mmiliki huyo kununua gesi moja kwa moja kutoka TPDC kwa kuwa ni chombo cha serikali badala ya kutumia watu wa kati ambao nia yao ni kutengeneza faida pekee na kusema kampuni iliyoingia kati kutaka kuwa kiunganishi wa kupata gesi kiwanda hicho, itafutiliwa mbali.
Kuhusu makaa ya mawe jasi (gypsum) Rais Magufuli alisema rasilimali hizo zipo hapa nchini na na kwamba nchi za Congo na Rwanda wananunua malighafi hizo hadi kwenye viwanda vyao na kwamba kiwanda cha Dangote kiko umbali wa kilomita mbili tu kutoka yaliko makaa hayo hivyo na makaa yenyewe ni bora na yanauzwa bei nafuu kuliko kuagiza kutoka nje.
Rais Magufuli amemuhakikishia mmiliki wa kiwanda hicho, Aliko Dangote kuwa serikali itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji na kumtaka mmiliki huyo kununua gesi moja kwa moja kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), badala ya kutumia watu wenye nia ya kutengeneza faida binafsi.
Rais Magufuli alisema hayo jana Ikulu jijini Dar es Salaam wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Dangote na kusema hakukuwa na tatizo lolote la kiserikali baina ya mwekezaji huyo, bali kulikuwa na watu waliotaka kujinufaisha binafsi kupitia mradi huo.
“Hakuna tatizo lolote baina ya serikali na mmiliki wa kiwanda hiki, bali kulikuwa na watu waliotaka kujinufaisha binafsi kupitia mradi huu kwa kufanya biashara za ujanja ujanja jambo ambalo serikali haliruhusu, na tutawachukulia hatua wote,”alisema Rais Magufuli.
Alisema mradi huo uliingiliwa na wapiga dili wakiwemo wanasiasa na kusema serikali haitaruhusu michezo hiyo na kwamba mianya yao imefungwa na wote waliohusika kutaka kuuvuruga, watashughulikiwa na serikali.
Rais Magufuli alimueleza mmiliki huyo nia ya serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inatimiza malengo ya kuwa nchi ya viwanda na kuwa iwapo atataka maelezo yoyote au iwapo atakwamishwa ni vyema awasiliane na viongozi wa serikali badala ya kutumia watu ambao nia yao ni kutengeneza faida tu.
“Iwapo unataka maelezo yoyote ama lolote linalokukwamisha uwasiliane na viongozi wa serikali badala ya kuwasiliana na watu ambao wako kwa ajili ya kufanya biashara ya ujanja ujanja kwa lengo la kupiga dili,” alisema Rais Magufuli.
Alisema mmiliki huyo alitaka eneo dogo kwa ajili ya kusafirishia saruji yake ila walijitokeza watu ambao wametaka kumuuzia kwa shilingi bilioni 43, jambo ambalo halina uhalisia wowote bali ni watu wenye nia ya kutaka faida na kusema jambo hilo haliwezekani katika serikali yake.
Akizungumzia hilo la eneo, Rais alisema wapo watu waliosikia Dangote anataka kununua eneo hilo dogo kwa ajili ya kusafirisha saruji na wao wakakimbilia kununua maeneo hayo na kutaka wamuuzie kwa bei kubwa, jambo ambalo alisema halikubaliki hata kidogo.
Kuhusu gesi Rais alimtaka mmiliki huyo kununua gesi moja kwa moja kutoka TPDC kwa kuwa ni chombo cha serikali badala ya kutumia watu wa kati ambao nia yao ni kutengeneza faida pekee na kusema kampuni iliyoingia kati kutaka kuwa kiunganishi wa kupata gesi kiwanda hicho, itafutiliwa mbali.
Kuhusu makaa ya mawe jasi (gypsum) Rais Magufuli alisema rasilimali hizo zipo hapa nchini na na kwamba nchi za Congo na Rwanda wananunua malighafi hizo hadi kwenye viwanda vyao na kwamba kiwanda cha Dangote kiko umbali wa kilomita mbili tu kutoka yaliko makaa hayo hivyo na makaa yenyewe ni bora na yanauzwa bei nafuu kuliko kuagiza kutoka nje.
Source:habarileo
Jiunge na hatukwamii.blogspot.com/ sasa
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video
0 comments:
Post a Comment