Wednesday, October 5, 2016

MONASTAR AMTOLEA POVU SHILOLE, KISA KIPO HAPA


Monastar ni mmoja wa wasanii waliokuwa chini ya kile alichokiita bendi ya shilole ambapo walikuwa wasanii 3, yani ni Monastar,Gaucho na Amadai.
Kilichotokea ni kuwa mambo yameenda kinyume na makubaliano yao, Kwa mujibu wa Mona.
Mona anasema kwamba walikubaliana na shilole kuwa atakuwa akienda nao kwenye show zake zote na kabla hajapanda jukwaani angewatanguliza wao jambo ambalo amelifanya mara kadhaa kwenye show za Dar es salaam.
Mona ameiambia Planet Bongo ya EA radio kuwa ghafla mambo yalianza kubadilika na Shishi akaanza kumpendelea zaidi mmoja wao ambaye ni Amadai.

Huyu amadai ndiye yule ambaye kulikuwa na
tetesi anatoka kimapenzi na Shilole. Hata hvyo mona alikataa kuzungumzia issue ya mahusiano ya wawili hao akisema ni mambo yao private ila ambacho hajaridhishwa nacho ni shilole kwenda kufanya show mikoani akiwa na amadai peke yake.
Mona Amesema, wamefanya kazi muda mrefu na makubaliano yao yalikuwa waondoke wote watatu kwenye mikoa yote alipopata show lakini dakika za mwisho wakashtukia amesepa na amadai.


0 comments:

Post a Comment