Monday, October 17, 2016

B.O.T- MZUNGUKO WA FEDHA NCHINI NI MDOGO

MZUNGUKO wa fedha katika uchumi wa Tanzania, umeporomoka kwa kasi katika kipindi kifupi tangu kuingia madarakani kwa Serikali ya Awamu ya Tano na kuathiri ukuaji uchumi karibu katika kila sekta.

Ripoti ya kila mwezi ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iliyotolewa hivi karibuni, ilieleza kuwa mzunguko huo wa fedha, ambao huchangia kujenga uwezo wa ununuzi katika uchumi, umefikia kiwango ambacho hakijawahi kutokea tangu mwaka 2012.



Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Desemba mwaka jana, mzunguko huo kwa maana ya noti na sarafu mikononi mwa watu na kwenye akaunti za watu benki, ulikuwa asilimia 18.8 lakini uliporomoka na kufikia asilimia 6.7 Julai.

Hali hiyo ilitajwa na ripoti hiyo ya Agosti, kuwa imechangiwa pamoja na mambo mengine, na hatua ya benki za biashara kupunguza utoaji mikopo kwa karibu kila sekta muhimu ya uchumi, kutokana na sekta hizo kushindwa kurejesha mikopo.

Sekta zilizoathirika

BoT imekiri kuwa utoaji mikopo katika sekta binafsi ambayo ndiyo injini ya uchumi, umeshuka kutoka asilimia 23.5 Julai mwaka jana hadi asilimia 15.2 Julai mwaka huu.

Hali mbaya zaidi kwa mujibu wa ripoti hiyo, imeonekana katika sekta za ujenzi, uzalishaji viwandani na hoteli na migahawa.

Katika ujenzi, BoT ilionesha kuwa Julai mwaka jana mikopo iliyotolewa kwenda sekta hiyo ilikuwa asilimia 22.9 ya mikopo yote, lakini Julai sekta hiyo iliambulia chini ya asilimia sifuri ya mikopo yote kwa kupata asilimia -4.

Sekta ya uzalishaji viwandani, BoT ilieleza kuwa mikopo imeshuka kutoka asilimia 30.7 Julai mwaka jana hadi chini ya asilimia sifuri, yaani asilimia -0.7 Julai mwaka huu; huku sekta ya hoteli na migahahawa utoaji mikopo ukitoka asilimia 13.6 Julai mwaka jana mpaka asilimia -0.4 Julai mwaka huu.


Bymtembezi


Jiunge na hatukwamii.blogspot.com/ sasa

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video 





0 comments:

Post a Comment