Sunday, April 23, 2017

‘Hatuihofii Simba’ – Juma Mwambusi

KOCHA msaidizi wa Yanga Juma Mwambusi amesema hawahofii timu yoyote watakayo kutanana nayo katika nusu fainali ya michuano ya Azam Sports Federation Cup.
Yanga ilipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Tanzania Prisons kwenye mchezo wa Kombe la FA, uliochezwa jana katika Uwanja Wa Taifa.
“Sisi ndiyo mabingwa watetezi wa kombe hili na tumejipanga kuhakikisha tunalitetea taji letu kwa nguvu zote, lakini tunajua timu zilizofika hatua hii ni bora lakini hatuihofii yoyote kama vile Simba, Azam, Mbao,” amesema Mwambusi.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mchezo huo kumalizika, kocha Mwambusi amesema, wachezaji wa timu zote mbili walicheza vizuri lakini mvua ilionekana kama kikwazo kwa wachezaji kutocheza kabumbu safi.
Timu yoyote itakayotwaa taji hilo itaiwakilisha nchi katika michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika ni kwa mujibu wa kanuni za Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF).
source:shaffihdauda
Tuandikie Maoni Yako Hapa Chini. Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video za kufurahisha na kuvunja mbavu.

0 comments:

Post a Comment