Thursday, October 6, 2016

BENKI YA DUNIA YAITAHADHARISHA TZ


The International Bank for Reconstruction and Development -IBRD (BENKI YA DUNIA), katika ripoti yake mpya imeitaja Tanzania kuwa ni miongoni mwa nchi 10 katika Bara la Afrika ambazo uchumi wake unakuwa kwa kasi, lakini imeonya kuwa kunahitajika juhudi za makusudi katika kuhakikisha kuwa ukuaji huo uzingatie mgawanyo wa kinachopatikana wenye kuleta ustawi na kupunguza kiwango cha utofauti wa matajiri na maskini.
Katika Taarifa yake hiyo, Benki ya Dunia imeitaka Tanzania kuwa na msukumo mpya katika kukabiliana na hali ya kutokuwa na usawa wa kiuchumi pamoja na Takwimu za miaka kumi mfululizo kuonesha zipo juu, bado hali ya wananchi haijakombolewa kutoka kwenye lindi kubwa la umaskini.

Read More

0 comments:

Post a Comment