Thursday, June 1, 2017

Real Madrid na Manchester United waoneshana ubabe kifedha.

Hiki ni kiburi kikubwa ambacho United wameamua kuwaonesha Real Madrid, ni sawa na kusema United hawataki chochote kile toka kwa Real Madrid bali wanataka waachane na wachezaji wao.
Dau la £60m ambalo Real Madrid wamelituma kwa Manchester United kumtaka David De Gea ni kubwa sana haswa kwa nafasi anayocheza David De Gea na ni wazi hii ilikuja kama bahati.
Lakini huwezi kuamini kwani Manchester United wamesema hapana na hawako tayari kupokea kiasi hicho cha fedha kwani David De Gea hauzwi kwa kiasi chochote kile na mpango wao ni abaki klabuni hapo.
Haitakuwa rahisi kwa Real Madrid kukubali kushindwa kwani ni timu ambayo mara zote imekuwa kama inahitaji mchezaji yoyote yule huwa wanamchukua hata kwa gharama kiasi gani.
Na David De Gea amekuwa mchezaji ambaye wanamtaka sana na kwa hakika watarudi tena na ofa mpya ambayo wanahisi inaweza kuishawishi United kumuuza De Gea.
source:shaffihdauda
Tuandikie Maoni Yako Hapa Chini. Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video za kufurahisha na kuvunja mbavu.

0 comments:

Post a Comment