Thursday, October 27, 2016

MADIWANI ARUSHA WAPATA MTETEZI


Sakata la posho za madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Arusha halijapoa, baada ya Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema) kuliibulia kwenye Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (Laac), akisema linakwamisha ukusanyaji wa mapato.

Selasini aliibua suala hilo jana wakati kamati ilipopitia na kuhoji hesabu za halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2014/15.

Alisema halmashauri hiyo imekata posho kwa madiwani na  watendaji na kuzipeleka fedha kwa walimu, jambo ambalo linawavunja moyo  wawakilishi hao wa wananchi kutimiza majukumu yao.



Source: mtembezi

Jiunge na hatukwamii.blogspot.com/ sasa

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video



0 comments:

Post a Comment