Friday, October 28, 2016

Kikwete achoshwa kulishwa maneno mtandaoni ‘nimestaafu niachwe nipumzike’


Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete ameelezea masikitiko yake juu ya matumizi mabaya ya picha zake mitandaoni.

Kikwete ambaye alikuwa Rais wa awamu ya nne, kupitia ukurasa wake wa twitter amesema watu wamekuwa wakitumia picha hizo katika mambo yao yakisiasa.
“Nasikitishwa sana na matumizi mabaya ya picha zangu mtandaoni hususan watu kunilisha maneno kwa kutaka kutimiza malengo yao ya kisiasa,” aliandika twitter.
Aliongeza, “Nimestaafu naomba niachwe nipumzike. Nisingependwa kuhusishwa na siasa za mtandaoni dhidi ya Serikali. Namuunga mkono Rais na Serikali yake,”.



Source: bongo5

Jiunge na hatukwamii.blogspot.com/ sasa

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video





0 comments:

Post a Comment