Tuesday, June 6, 2017

Hili ndio chama bora la CHAMPIONS LEAGUE.

Baada ya fainali ya Champions League kupigwa na Real Madrid kubeba kikombe hicho sasa kikosi bora katika mashindano hayo msimu huu kimeshatajwa huku majina makubwa kama Neymar,Suarez na Paulo Dyabala yakikosekana.
Katika kikosi hicho golikipa wa Juventus Gianluig Buffon amekuwa kipa namba moja wa kikosi hicho huku akisaidiwa na mlinda mlango wa klabu ya Atletico Madrid Jan Oblak.
Katika walinzi yumo mlinzi wa kati wa klabu ya Juventus Leornado Bonnucci huku walinzi watatu wa Real Madrid Sergio Ramos,Marcelo na Dani Carvajal wakiwepo eneo la ulinzi huku mlinzi wa Atletico Madrid Diego Godin naye pia akiwepo.
Katika eneo la kiungo, wachezaji wanne kati ya sita waliochaguliwa katika nafasi hiyo ya kiungo wanatokea Real Madrid ambao ni Casemiro,Modric,Isco na Toni Kroos huku Miralem Pjanic wa Juventus na Tiemoue Bakayoko wa Monaco nao wakiwemo katika kikosi hiki
Katika nafasi ya ushambuliaji Cristiano Ronaldo,Lioneil Messi na Antoine Griezman wapo katila kikosi hicho huku bwanamdogo Kylian Mbappe wa Monaco na Robert Lewandoski wa Bayern Munich nao wakiwepo katika eneo la ushambuliaji.
source:shaffihdauda
Tuandikie Maoni Yako Hapa Chini. Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video za kufurahisha na kuvunja mbavu.

0 comments:

Post a Comment