Thursday, August 10, 2017

Chicharito atashangilia akiifunga United? Hili hapa jibu lake

Javier Hernandez “Chicharito” ni moja kati ya wachezaji vya mashabiki wa Manchester United na hata alipouzwa na Louis Van Gaal wengi walisikitika sana.
Wikiendi hii Chicharito anarudi Old Trafford lakini safari hii akiwa mpinzani wa Manchester United kwani atakuwa amevaa uzi wa wagonga wa London klabu ya West Ham.
Ni utaratibu wa wachezaji wengi wanapozifunga timu zao za zamani kutoshangilia goli, lakini je kwa Chicharito itakuwaje kama akiifunga Manchester United?
“Ni klabu yangu ya zamani, mashabiki wa zamani na uwanja wa zamani il pia kama nikifunga litakuwa bao langu la kwanza kwa West Ham kwa sasa sijawaza kuhusu kushangilia” alisema Chicharito.
Inaonekana kama vile mshambuliaji huyo amepania kuifunga United kwani amesisitiza kuwa kufunga katika mechi ya kwanza litakuwa jambo zuri sana kwa upande wake. United na West Ham zitapambana siku ya Jumapili katika ufunguzi wa Epl.

Tuandikie Maoni Yako Hapa Chini. Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video za kufurahisha na kuvunja mbavu.

0 comments:

Post a Comment