Thursday, July 27, 2017

Makamba kushuhudia robo fainali Ndondo Cup Power Breakfast vs Amplifier

Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais na Mazingira Mh. January Makamba leo Julai 27, 2017 atakuwa mgeni rasmi kwenye michuano ya Ndondo Cup ambapo atashuhudia mchezo wa kwanza wa hatua ya robo fainali.
Mchezo huo utakuwa kati ya Vijana Rangers ambao wako chini ya kipindi cha Amplifier kinachoongozwa na watangazazi Millard Ayo na Meena Ally dhidi ya Kibada One chini ya Power Breakfast chini ya Babra Hassan, Masoud Kipanya PJ na wengine.
Mechi itachezwa kwenye uwanja wa Kinesi saa 10:00 jioni na itaoneshwa live kupitia Azam TV.
source:shaffihdauda
Tuandikie Maoni Yako Hapa Chini. Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video za kufurahisha na kuvunja mbavu.

0 comments:

Post a Comment