Saturday, October 29, 2016

emi Alade, Chameleone na Tekno kuungana na mastaa wa Bongo kwenye Fiesta ya Dar

Yemi Alade alishinda tuzo ya msanii bora wa kike, na Tekno akachukua ya msanii bora aliyechipukia kwenye tuzo za MTV MAMA 2016 – hawa wawili hawakwepeki na hakuna ubishi ni miongoni mwa wasanii wa moto zaidi Afrika kwa sasa.

Wapopo hao wametajwa kutumbuiza kwenye kilele cha tamasha la Fiesta, litakalofanyika jijini Dar kwenye viwanja vya Leaders, November 5.
Hiyo sio mara ya kwanza wawili hao kuja Dar. Supastaa na nguli wa muziki wa Uganda, Jose Chameleone naye atatumbuiza kwenye show hiyo.
Wasanii wengine watakaopanda jukwaani siku hiyo ni pamoja na Alikiba, Raymond, Mr Blue, Belle 9 ba wengine. Bado haijajulikana ni msanii yupi kutoka Marekani atakayetumbuiza mwaka huu.

Source: bongo5

Jiunge na hatukwamii.blogspot.com/ sasa

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video





0 comments:

Post a Comment